Wednesday, 4 March 2015

JE WATAKA KUVUKA NA KUTAWALA




Watu wengi tunajua ya kuwa MUNGU alituumba ili tumilki  na kutawala. Kitu kilicho sababisha hata sasa hatufanikwi ni kule kutotii sauti ya MUNGU na jambo hili limefanya watu kutosonga mbele kimaisha maana neno la MUNGU linasema katika  Joshua 1:8 Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku upate kuangalia na kutenda sawaswa na maneno yote  yaliyoandikwa humo, maana ndipo utakapofanikisha njia yako kisha ndipo utakapostawi sana.
Je ndani yako ndani yako kunalo neno la Mungu? Wakristo wengi wamejisahau hata kusoma neno la MUNGU, unakuta mkristo muda mwingi yuko WhatsAp, Facebook, wasengenyaji n.k. Na watu hawa ndio mara nyingi utawaona wako rohoni kumbe hao ndio waharibifu wa kazi ya MUNGU.  Watu wengi wanajikuta wamewaamini  hawa watu na kuwapa mambo yao ya siri halafu  wanayakuta yamezagaa mitaani wasijue kua Siri zao wamepeleka sehemu isiyo sahihi. Sababu kuwa  mwana wa MUNGU nikuwa mbeba siri za MUNGU kwa hiyo watu hawa wamekuwa kidonda katika kazi ya Mungu na hii imekua ikurudisha nyuma kazi ya MUNGU.
 Na watu hawa wamekuwa wakipatwa  na magonjwa yanayo sababishwa na uchungu wa ndani (yaani lile jambo ulilolibeba moyoni ). Biblia inasema MITHALI 14:30a Moyo  ulio mzima ni uhai wa mwili . Je hawa wapendwa feki wanaua watu wangapi kwenye makanisa wanayosali? Kama na wewe upo katika kundi hilo tambua biblia inasema katika Luka17:2 Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini,  kuliko kumkosesha mmoja wa wadogo hawa. Je kunayo sababu ya wewe kusema kuwa nimeokoka! badilika tambua kuwa unavyofanya MUNGU hapendezwi na wewe na shetani anakushangaa.
Tambua kuwa bado unayo nafasi ya kutengeneza na Bwana MUNGU wako,  nenda mbele za MUNGU mwabie baba nimekosa tamka makosa yako bila kuficha mbele za MUNGU sababu  Mithali 11:7 inasema Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea; na matumaini ya uovu huangamia. Kwahiyo inapasa kuungama dhambi zote.Wala Usiache hata moja kwa kuhofia watu wanasikia  endelea kumsihi MUNGU wako naye atakusamehe.
Ukisoma ZABURI 51:7 Unisafishe kwa hisopo nami nitakuwa safi,  Unioshe, nami nitakuwa mweupe kama theluji, hii ina maana kwamba dhambi zako zitakuwa mbali na wewe  na wakati huo utaanza kuisikia sauti ya MUNGU ikikuongoza katika Jina lipitalo majina yote, jina la YESU.
 MUNGU AWABARIKI KWA KUWEZA KUTUMIA MUDA WAKO KUJIPATIA UFAHAMU KATIKA NENO LA MUNGU
MTUMISHI FRANK MINJA.

Saturday, 28 February 2015

SOMA KWA AJILI YAKO NDANI YA KRISTO

Bwana Yesu asifiwe tunawamshukuru wale wote waliotembelea ukurasa wetu na blog hii ya KILIMANJARO HOUSE OF PRAYER,
 Tunapenda kuwataarifu kwamba hili sio kanisa bali ni mahali tu tumejitolea ili tuweze kukutanika kwa ajili ya  maombi na si vinginevyo, Tunajua umuhimu wa maombi katika maisha ya mwanadamu awaye yeyote anayeishi duniani hivyo kwa Mwongozo wa ROHO MTAKATIFU ndio tukaona tushirikishane jambo hili la Baraka katika maisha ya kila siku duniani.
Jambo hili limekuwa jema na Mungu atupaye uwezo wa kufanya makuu siku zote atusaidie sote ili shetani asituvuruge wala kuleta uhasama kati ya madhehebu na makanisa.
Tuongozwe na Roho kama Neno la MUNGU wetu linavyotuagiza katika WAGALATIA 5:25, na WAEFESO 6:10-12, jambo lililo jema watumishi wa Mungu tuelewane na tumpinge shetani na zaidi sana tusikamane kuujenga mwili wa Kristo Yesu Bwana wetu na tukizidi kuombeana kwa kusudi la kuwakamilisha WATAKATIFU ambalo ndilo hasa lengo la Mungu kwa kanisa.

MUNGU WA MBINGUNI AZIDI KUWABARIKI KILA MMOJA NA KUMPA KILA MMOJA HEKIMA YA KUTENDA SAWA NA NENO LINAVYOTUAGIZA KATIKA BIBLIA, ILI SIKU MOJA TUKAPEWE TAJI TUKIWA MASHUJAA TULIOSHINDA VITA VYA KIROHO HAPA DUNIANI.
Endeleeni kutembelea ukurasa wetu na pia mtoe maoni kile ambacho kitakuwa chema zaidi kwa kusudi la Ufalme.AEN.

Tuesday, 24 February 2015

           

 WELCOME AT KILIMANJARO HOUSE OF PRAYER.

 

 

 

   KILIMANJARO HOUSE OF PRAYER

Kilimanjaro House of Prayer is the Prayer Center which located at Kiboroloni, Moshi Kilimanjaro, is where the people of God comes together and Pray to Almighty God.