Saturday, 28 February 2015

SOMA KWA AJILI YAKO NDANI YA KRISTO

Bwana Yesu asifiwe tunawamshukuru wale wote waliotembelea ukurasa wetu na blog hii ya KILIMANJARO HOUSE OF PRAYER,
 Tunapenda kuwataarifu kwamba hili sio kanisa bali ni mahali tu tumejitolea ili tuweze kukutanika kwa ajili ya  maombi na si vinginevyo, Tunajua umuhimu wa maombi katika maisha ya mwanadamu awaye yeyote anayeishi duniani hivyo kwa Mwongozo wa ROHO MTAKATIFU ndio tukaona tushirikishane jambo hili la Baraka katika maisha ya kila siku duniani.
Jambo hili limekuwa jema na Mungu atupaye uwezo wa kufanya makuu siku zote atusaidie sote ili shetani asituvuruge wala kuleta uhasama kati ya madhehebu na makanisa.
Tuongozwe na Roho kama Neno la MUNGU wetu linavyotuagiza katika WAGALATIA 5:25, na WAEFESO 6:10-12, jambo lililo jema watumishi wa Mungu tuelewane na tumpinge shetani na zaidi sana tusikamane kuujenga mwili wa Kristo Yesu Bwana wetu na tukizidi kuombeana kwa kusudi la kuwakamilisha WATAKATIFU ambalo ndilo hasa lengo la Mungu kwa kanisa.

MUNGU WA MBINGUNI AZIDI KUWABARIKI KILA MMOJA NA KUMPA KILA MMOJA HEKIMA YA KUTENDA SAWA NA NENO LINAVYOTUAGIZA KATIKA BIBLIA, ILI SIKU MOJA TUKAPEWE TAJI TUKIWA MASHUJAA TULIOSHINDA VITA VYA KIROHO HAPA DUNIANI.
Endeleeni kutembelea ukurasa wetu na pia mtoe maoni kile ambacho kitakuwa chema zaidi kwa kusudi la Ufalme.AEN.

Tuesday, 24 February 2015

           

 WELCOME AT KILIMANJARO HOUSE OF PRAYER.

 

 

 

   KILIMANJARO HOUSE OF PRAYER

Kilimanjaro House of Prayer is the Prayer Center which located at Kiboroloni, Moshi Kilimanjaro, is where the people of God comes together and Pray to Almighty God.